Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 7 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 53 2021-04-12

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza:-

Uziwi ni moja ya aina ya ulemavu ambao una lugha yake ya ishara (signal language).

(a) Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kufundisha Lugha ya Ishara kama moja ya masomo ya lazima Shuleni kwa wanafunzi wote kuanzia Elimu ya Awali ili kuondoa kikwazo cha mawasiliano kati ya wenye uziwi na wale wanaosikia?

(b) Je, Tanzania tuna vitabu vya kufundishia Lugha ya Ishara katika lugha ipi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Stephen Lemomo Kiruswa Mbunge Longido, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Lugha ya alama katika kuondoa kikwazo cha mawasiliano kati ya wenye uziwi na wale wasio na uziwi. Aidha, ili kufikia lengo la kufundisha lugha ya alama kama somo katika ngazi zote za elimu, Serikali imechukua hatua mbalimbali za kuboresha ufundishaji wa lugha hiyo. Hatua hizo ni pamoja na kukamilika kwa usanifishaji wa Kamusi ya Lugha ya Alama ya Tanzania pamoja na uandaaji wa Mwongozo wa Utekelezaji wa Mtaala wa Elimu ya Sekondari kwa wanafunzi viziwi Kidato cha kwanza mpaka cha nne chini ya Taasisi ya Elimu Tanzania.

Mheshimiwa Spika, vile vile, kupitia Chuo cha Ualimu Patandi na Chuo Kikuu cha Dodoma walimu wenye taaluma ya Elimu Maalumu katika fani ya ukiziwi na lugha ya alama wanaandaliwa.

Mheshimiwa Spika, vitabu vinavyotumika kufundishia lugha ya Ishara vimeandikwa katika lugha ya Kiingereza na Kiswahili ili kukidhi mahitaji ya ufundishaji na ujifunzaji. Ahsante.