Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 6 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 48 2021-04-09

Name

Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Primary Question

MHE. ALI HASSAN OMAR KING aliuliza:-

Je, wizi unapotokea kwenye akaunti ya benki ya mteja uliofanywa na mtumishi wa benki ni nani mwenye wajibu wa kumlipa mteja?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ali Hassan Omar King, Mbunge wa Jang’ombe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, wizi unapotokea kwenye akaunti ya benki ya mteja, uchunguzi wa kina hufanywa na vyombo husika katika masuala ya upelelezi ikiwa ni pamoja na Jeshi la Polisi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa kadri hali na mazingira ya tukio yatakavyokuwa yametokea.

Mheshimiwa Naibu Spika, endapo ikibainika kuwa wizi huo umefanywa na mtumishi wa benki, hatua stahiki huchukuliwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo ikiwa ni pamoja na mteja kulipwa kiasi cha fedha alichoibiwa na mhalifu kuchukuliwa hatua za kinidhamu pamoja na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. Pia, Benki Kuu hutoa adhabu kwa benki husika pale inapobainika kwamba utaratibu uliowekwa na benki husika ulikuwa na kasoro zilizochangia kuibiwa kwa fedha za mteja.