Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 16 Good Governance Ofisi ya Rais TAMISEMI. 131 2016-05-10

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-
Tangu kuanzishwa kwa Wilaya ya Mbogwe mwaka 2012 watumishi iliyokuwa Wilaya ya Bukombe walihamishiwa Wilayani Mbogwe lakini hawajalipwa stahiki zao za posho ya kujikimu pamoja na zile za usumbufu.
Je, ni lini watumishi hao watalipwa stahiki zao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, idadi ya watumishi waliohamishwa kutoka Wilaya ya Bukombe kwenda Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe ni 73 ambao wanadai posho ya kujikimu na usumbufu ya shilingi milioni 164.14. Kati ya madai hayo fedha ambazo zimeshalipwa kwa watumishi ni shilingi milioni 15.15 kwa watumishi 18. Hivyo, kiasi ambacho watumishi bado wanadia shilingi 148. 99.
Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka 2016/2017, Halmashauri imeomba fedha hizo katika Wizara ya Fedha na Mipango ili kulipa deni hilo kwa watumisi 55 waliobaki. Ofisi ya Rais, TAMISEMI itaendelea kufuatilia Hazina fedha hizo ili ziweze kupatikana na kulipwa kwa watumishi wanaodai.