Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 70 2021-09-07

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI H. XADAY aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kituo cha kupooza umeme Mjini Katesh kwani kuna line ndefu ya Km 780 hivyo kusababisha umeme kukatika mara kwa mara Wilayani Hanang?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI aljibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Samwel Hhayuma Xaday, Mbunge wa Hanang, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) limeanza taratibu za ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme pamoja na kituo kidogo (switching yard) cha kilovoti 33 kutoka njia kuu ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 400 inayoendelea kujengwa kutoka Singida hadi Namanga katika Kijiji cha Mogitu Wilayani Hanang.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa kituo hicho utaboresha hali ya upatikanaji wa umeme katika maeneo ya Wilaya ya Hanang na maeneo jirani utaanza mwezi Julai, 2022 na kukamilika Juni, 2023. Gharama ya mradi ni takribani shilingi bilioni 2.6. Utekelezaji wa mradi huu utagharamiwa na Serikali kwa asilimia 100.