Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 50 2021-09-03

Name

Abdulhafar Idrissa Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtoni

Primary Question

MHE. ABDUL- HAFAR IDRISSA JUMA Aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukifungua Kituo cha Polisi cha Betrasi kilichopo katika Jimbo la Mtoni Zanzibar ambacho kimefungwa kwa zaidi ya mwaka sasa?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI, Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdul-Hafar Idrisa Juma Mbunge wa Mtoni Zanzibar, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Polisi cha Betrasi ni kituo kidogo cha polisi ambacho kilijengwa mwaka 1994 na kilikuwa kinafanya kazi kwa masaa 12, kutwa na kilikuwa kinawahudumia wananchi wa eneo la Mtoni na kilijengwa na mdau wa ulinzi kwa wakati ule Ndugu Noushad Mohamed. Kituo hiki kilifungwa mwaka 2018 kutokana na uhaba wa askari. Wananchi wa eneo hilo pia wanapata huduma za polisi katika Kituo cha Polisi cha Bububu na pindi pakipatikana ongezeko la askari kituo hicho pamoja na vituo vingine vya aina hiyo vitafunguliwa ili kuhudumia wananchi. Nakushukuru.