Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 49 2021-09-03

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA Aliuliza:-

Je, Serikali ilishawahi kulifanyia matengenezo yoyote muhimu gari lililotolewa na Mbunge kutoka kwa wafadhili toka Japan na kupelekwa Kituo cha Polisi Gonja katika Jimbo la Same Mashariki mwaka 2015?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi naomba ama napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela Mbunge wa Same Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimwa Naibu Spika, Kituo cha Polisi cha Gonja kilichopo Wilaya ya Same kina gari namba PT 1988 Toyota Land Cruiser, ambalo lililetwa hapo mnamo mwaka 2015 ili kuhudumia wananchi. Mnamo tarehe 22 Juni, 2021 gari hilo lilisimama kufanya kazi ili kulinda usalama wa watumiaji na katika kulifanyia ukaguzi gari hilo lilikutwa lina ubovu wa mfumo wa usukani, mfumo wa break, clutch plate, mfumo wa umeme, ball joints na kuisha kwa matairi na bush. Aidha, tathmini ya matengenezo ya gari hilo ni shilingi 4,500,000 na fedha za matengenezo zimeshaombwa kutoka Makao Makuu ya Polisi. Ninakushukuru.