Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 4 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 48 2021-09-03

Name

Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN Aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wa kulisaidia kwa kulijengea uwezo Jeshi la Kujenga Uchumi la Zanzibar (JKU)?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nijibu swali la Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan, Mbunge wa Chake Chake kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mashirikiano kati ya JKT na JKU yalianza mwaka 1975, kuanzishwa kwa JKU kutoka mfumo wa kambi za vijana ulioanzishwa tarehe 3 Machi, 1965 kwa sehemu kubwa kulitokana na mashirikiano hayo. Tangu wakati huo JKT na JKU wameendelea kubadilishana uzoefu katika maeneo mbalimbali ya kiutawala na uzalishaji mali na ndiyo maana JKU ina sura ya JKT. Mwaka 2001 iliundwa Kamati ya Mashirikiano yaliyopelekea kuwa na Katiba ya Mashirikiano ya mwaka 2007. Katiba hiyo pamoja na mambo mengine imeainisha vikao mbalimbali vya mashirikiano ikiwa ni pamoja na ratiba za vikao vya wakuu wa vyombo hivyo.