Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 3 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 34 2021-09-02

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA Aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaendeleza kimasomo watoto wa kike waliokatisha masomo kwa kupata ujauzito?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kuwaendeleza wanafunzi wanaoacha masomo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo wasichana waliopata ujauzito. Mikakati hiyo ni pamoja na Mpango wa Elimu Nje ya Mfumo Rasmi. Katika mpango huu wanafunzi wanaruhusiwa kufanya mitihani ya Kidato IV na cha VI. Kwa sasa kuna Vituo 753 vya Elimu nje ya mfumo rasmi vilivyosambaa katika mikoa yote ya Tanzania Bara.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hiyo, Serikali imeendelea kutoa fursa za wanafunzi kujiendeleza wakiwemo wale waliopata ujauzito. Fursa hizo ni pamoja na:- Mpango wa Elimu ya Msingi kwa walioikosa (MEMKWA), mpango wa elimu kwa vijana uitwao Elimu Changamani kwa Vijana Walio Nje ya Shule (Integrated Program for Out of School Adolescents - IPOSA). Serikali pia inatoa fursa za kujiendeleza kupitia Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (FDC) ambapo maeneo Manne ambayo ni; Taaluma (Academic skills), Stadi za Ufundi wa awali (pre-vocational skills), Ujasiriamali na Stadi za maisha (Generic Skills) kusisitizwa katika ujifunzaji. Ahsante.