Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 2 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 29 2021-09-01

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO Aliuliza:-

(a) Je, ni kwa nini Jeshi la Wananchi wa Tanzania lisifuate utaratibu, ili kumiliki eneo la wananchi wa Kitongoji cha Byawamala, Kijiji cha Bulifani, katika Kata ya Kyaka, badala ya kuhamia eneo hilo kwa nguvu na hivyo kuibua mgogoro kuhusu eneo hilo?

(b) Je, ni kwa nini eneo hilo lisigawanywe kwa Jeshi na Wananchi kwa kuwa eneo hilo ni kubwa na limekuwa pori kwa sasa?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge wa Nkenge, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, eneo la jeshi linalotambulika kama Kiteule cha 21- KJ lipo Bulifani, Kyaka, Wilaya ya Misenyi. Eneo hili lilitumika wakati wa Vita vya Uganda kwa kujikinga na kuyashambulia majeshi ya Nduli Idd Amin Dada. Mpaka sasa eneo hilo bado lina mahandaki yaliyotumika wakati wa vita. Hivi sasa eneo hili linakaliwa na askari wetu na limekuwa Kiteule cha 21-KJ Kaboya.

Mheshimiwa Spika, mwezi Julai, 2021 timu ya wataalamu wa ardhi kutoka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa walikwenda kutembelea eneo hilo na kufanya tathmini ya uthamini na upimaji. Eneo hili litaingizwa kwenye mpango wa miaka mitatu ya kuondoa migogoro iliyopo katika maeneo yote ya jeshi, mpango ambao umeanza Aprili, 2021. Naomba wananchi wawe na subira katika kipindi hiki kifupi kilichobakia.

Mheshimiwa Spika, eneo hili halitaweza kugawanywa kwa wananchi kwa kuwa, lipo kwa matumizi ya jeshi na eneo hili limekaa kimkakati zaidi. Nakushukuru.