Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 13 2021-08-31

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI Aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kusambaza umeme katika Vijiji na Vitongoji kupitia REA III hasa katika maeneo ambayo nguzo zimetelekezwa barabarani zaidi ya miaka miwili?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuena Athumani Bushiri, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini - REA na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), inaendelea kutekeleza mpango wake wa kusambaza umeme vijijini awamu ya tatu, mzunguko wa pili katika vijiji vyote nchini. Utekelezaji wa mradi huu ulianza mwezi Machi, 2021 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Disemba, 2022.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Mradi huu unalenga kufikisha umeme katika vijiji 1,956 kati ya vijiji 12,268 ambavyo havijafikiwa na umeme. Kazi ya kupeleka umeme katika vitongoji ni endelevu inayoendelea kutekelezwa kupitia TANESCO na REA ikiwa ni kazi ya kuendelea kuunganisha huduma ya umeme kwa wananchi.