Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 5 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 34 2021-04-08

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU Aliuliza:-

(a) Je, ni lini Serikali itatekeleza kikamilifu Waraka Na. 3 wa mwaka 2015 kuhusu Muundo wa Kada ya Uhasibu na Ukaguzi wa Ndani?

(b) Je, ni lini Kitengo cha Uhasibu na Fedha katika Wizara na Sekretarieti za Mikoa zitapewa hadhi ya kuwa Idara?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwanza, naomba nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uzima pamoja na afya njema. Pia nitumie nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan kwa imani yake aliyokuwa nayo kwa kuniteua kuwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya shukrani hizo, naomba sasa kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, nijibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

(a) Mheshimiwa Spika, Waraka Na. 3 wa mwaka 2015 kuhusu Muundo wa Kada ya Uhasibu na Ukaguzi wa Ndani ulianza kutekelezwa mwezi Julai, 2018 kwa kutenganisha Kada ya Maafisa Hesabu na Wahasibu. Kwa mujibu wa muundo huo mpya Wahasibu na Wakaguzi ni wale ambao wana CPA na wale wasio na CPA wanatambulika kama Maafisa Hesabu na Maafisa Ukaguzi.

(b) Mheshimiwa Spika, kuhusu kupandisha hadhi vitengo vya uhasibu na fedha katika Wizara na Sekretarieti za Mikoa kuwa idara, katika kuandaa miundo ya taasisi, vigezo kadhaa hutumika ili kufikia maamuzi ya kuwa Idara, Vitengo na Sehemu. Kwa kuwa miundo hii hufanyiwa marekebisho mara kwa mara kwa kushirikiana na wataalamu wa miundo kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na kujadiliwa katika ngazi ya maamuzi, ni mategemeo yetu kwamba Serikali itakapoona kuwa Kitengo cha Uhasibu na Fedha kinakidhi vigezo vya kuwa idara, kitapewa hadhi hiyo.