Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 33 2021-04-08

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO Aliuliza:-

Jeshi la Polisi linashikilia pikipiki nyingi katika Vituo vya Polisi kwa muda mrefu.

(a) Je, Serikali haioni fedha nyingi zinapotea kwa pikipiki nyingi kuchakaa zikiwa katika Vituo vya Polisi na hivyo kuleta hasara kwa Taifa?

(b) Je, kwa nini Serikali isiunde Kamati Maalum kila baada ya miaka mitatu kupitia sababu zilizosababisha pikipiki hizo zishikiliwe kwa muda mrefu?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, sasa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vedastus Mathayo Manyinyi, Mbunge wa Musoma Mjini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pikipiki ni mojawapo ya chombo cha moto kinachotumika kufanya biashara ikiwemo kusafirisha watu kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine. Kuna sababu tatu zinazopelekea kushikiliwa kwa pikipiki hizo kwenye Vituo vya Polisi:-

(i) Kundi la kwanza, ni zile pikipiki zilizokamatwa kwenye makosa ya jinai ambazo zimetumika kwenye kutenda makosa au zilizoibiwa toka kwa watu;

(ii) Kundi la pili ni zile pikipiki zilizokamatwa baada ya kutenda makosa ya usalama barabarani; na

(iii) Kundi la tatu ni zile pikipiki zilizookotwa na hazina wenyewe na kuhifadhiwa vituoni. Hivyo pikipiki hizi zipo vituoni kama vielelezo vya kesi na vielelezo ambavyo havina mwenyewe na kuwepo kwake kituoni ni kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zilizopo.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kufuatilia kwa ukaribu mashauri yote yaliyopo Mahakamani yanayohusu vielelezo vilivyopo Vituo vya Polisi yamalizike kwa wakati ili mashauri hayo yasikae muda mrefu. Aidha, Pikipiki na vyombo vingine vya moto kuondolewa kwake vituoni kunategemea na amri ya Mahakama na maamuzi ya kesi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sasa tatizo hili si kubwa linahimilika, lakini iwapo tathmini itaonyesha kuongezeka ukubwa wa tatizo hili, basi Serikali ipo tayari kuunda Kamati Maalum kama ilivyoshauriwa na Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Spika asante.