Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 29 2021-04-06

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. KHATIB SAID HAJI Aliuliza:-

Je, Serikali inachukua hatua gani ya dharura kukabiliana na mrundikano mkubwa wa mahabusu katika magereza nchini?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi pia nichukue fursa hii kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu, lakini pia nimshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuwa na imani na sisi Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Khatib Said Haji, Mbunge wa Jimbo la Konde kutoka Mkoa wa Kaskazini Pemba, nalijibu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua uwepo wa changamoto ya msongamano wa wafungwa na mahabusu magerezani na imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kukabiliana na changamoto hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia tarehe 30 Machi, 2021 idadi ya wafungwa na mahabusu nchini ilikuwa ni 33,473 kati ya hao waliohukumiwa ni 16,735 na mahabusu ni 16,738 huku uwezo wa magereza yetu nchini ni kuhifadhi wafungwa na mahabusu 29,902.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kukabiliana na kutatua changamoto hizo Serikali imechukua baadhi ya hatua nyingi ambazo tunaamini kwa njia moja ama nyingine zinakwenda kutatua ama kuondoa kabisa tatizo hili la mlundikano wa mahabusu katika magereza.

Kwanza Serikali imeamua ama inaendeleza ushirikishwaji wa vyombo vya haki jinai, lakini kingine kufanya mabadiliko ya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2009, lakini pia ushirikishwaji wa Mahakama na Jeshi la Magereza katika kutumia mfumo wa TEHAMA (video conference), lakini kingine kufanya upanuzi na kujenga magereza mapya ya Wilaya ambazo hazikuwa na Magereza kama vile Chato na Ruangwa, lakini kingine utoaji wa dhamana kwa masharti nafuu, lakini pia kuanzishwa kwa mahakama zinazotembea (mobile court) kwa mashauri madogo madogo yanayotolewa uamuzi pasipo watuhumiwa kupelekwa magerezani. Aidha, kutoa elimu kwa raia ili, kutojihusisha na vitendo vya kihalifu, jambo ambalo linaweza kwa kiasi kikubwa likapunguza mlundikano wa mahabusu katika magereza. Ahsante. (Makofi)