Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 2 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 19 2021-03-31

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA Aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya sasa ya kurejesha mfumo wa TANePS Hazina ili ukatekelezwe na kusimamiwa pamoja na GePG katika kuongeza ufanisi?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO Alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jerry William Silaa, Mbunge wa Ukonga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mfumo wa TANePS umetayarishwa na kukidhi matakwa ya sheria ya ununuzi wa umma Sura Na. 410 ambayo imeweka misingi na taratibu za ununuzi wa umma inayohimiza uwazi, usawa na haki katika michakato ya ununuzi ili kuipatia Serikali thamani halisi ya fedha zinazotumika katika ununuzi wa bidhaa na huduma mbalimbali. Aidha, kifungu Na. 9(1) cha Sheria kimeipa nguvu mamlaka ya udhibiti wa ununuzi wa umma kuanzisha na kusimamia mifumo na taratibu zote zinazohusu masuala ya ununuzi wa umma ikiwa ni pamoja na mfumo wa TANePS.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa mfumo wa TANePS tayari umeunganishwa na mifumo ya GPG na taratibu zinaendelea ili kuunganisha na mifumo mingine ya Serikali ikiwemo mifumo ya MUSE na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Ununuzi wa Umma Sura Na. 410 pamoja na Kanuni zake, Serikali inaendelea kuboresha utendaji na mfumo TANePS ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za ununuzi, hivyo basi haioni haja ya kuhamishia mfumo huo Hazina kwa sasa. Ahsante.