Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 8 2021-03-30

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. REUBEN N. KWAGILWA Aliuliza:-

Je, ni lini wananchi katika mitaa 30 isiyo na umeme Wilayani Handenni watapatiwa umeme kulipia mradi wa REA?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Reubne Nhamanilo Kwagilwa Mbunge wa Handeni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TANESCO na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kutekeleza mradi wa kusambaza umeme katika vijiji, mitaa na vitongoji visivyokuwa na umeme kupiitia miradi mbalimbali. Kwa sasa mkandarasi Kampuni ya M/S Sengerema Engineering Ltd. amepewa kazi ya kupeleka umeme katika vijiji 15 na mitaa vitongoji zaidi ya 30 katika Wilaya ya Handeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi hizo zinajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa KV 0.4 umbali wa km. 27.5, ufungaji wa transfoma 11 za 50 kVA na 100 kVA; pamoja na kuwaunganisha wateja wa awali 669. Mradi unakadiriwa kugharimu shilingi bilioni 3.36. Utekelezaji wa mradi umeanza mwezi Februari, 2020 na utakamilika ifikapo Disemba, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, TANESCO inaendelea kuunganisha umeme kwa wateja ambao hawajaunganishiwa umeme katika mitaa na vitongoji vya Tanzania Bara ikiwemo Wilaya ya Handeni kupitia majukumu yake ya kila siku.