Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 7 2021-03-30

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI Aliuliza:-

Je, ni lini Daraja la Kisorya – Lugezi litakalounganisha Wilaya za Bunda na Ukerewe litajengwa ili kurahisisha ukuaji wa uchumi wa wananchi wa Wilaya hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa ujenzi wa daraja litakalounganisha Wilaya ya Bunge na Ukerewe ni sehemu ya mradi wa ujenzi wa barabara ya Nyamuswa – Bunda – Bulamba – Kisorya – Nansio yenye urefu wa kilomieta 121.6 ambao utekelezaji wake umeanza na uko katika hatua mbalimbali. Kazi ya upembuzi yakinifu na usaniifu wa kina wa barabara ya Nyamuswa – Bunda – Bulamba hadi Kisorya yenye urefu wa kilometa 107.1 ilikamilika Machi, 2013. Aidha, usanifu wa kina wa sehemu ya barabara ya Kisorya – Rugezi – Nansio (Ukerewe) yenye urefu wa kilometa 14.5 pamoja na Daraja la Rugenzi – Kisorya ulikamilika Aprili, 2017.

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi huu umegawanyika katika sehemu tatu, yaani Lots tatu, ambazo ni Nyamuswa – Bunda – Bulamba (Lot I) yenye urefu wa kilometa 56.1; Lot II bulamba – Kisorya yenye km. 51 na Lot III Kisorya – Lugezi – Nansio yenye urefu km. 14.5 inayojumuisha na daraja la Kisorya – Rugezi yaani daraja lina urefu wa mita 1000. Hadi sasa ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Bulamba – Kisorya ambao ni Lot II umekamilika. Ujenzi wa sehemu ya Nyamuswa – Bunda – Bulamba Lot I kwa kiwango cha lami unaendelea na umefikia asilimia tano. Aidha, ujenzi wa sehemu ya Rugezi – Nansio Pamoja na daraja la Kiisorya – Rugezi utaannza baada ya fedha kupatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi wa sehemu ya Kisorya – Rugezi – Nansio ikiwemo ujenzi wa daraja Serikali kupitia wakala wa ufundi na umeme TEMESA inaendelea kutoa huduma ya kuvusha wananchi wa maeneo haya kupitia kivuko cha MV Ujenzi.