Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 5 2021-03-30

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali italeta Mradi wa Kuhifadhi Mazingira Mufindi katika chanzo cha maji cha Mto Ruaha na shamba la miti la Sao Hill?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuhifadhi na kutunza vyanzo vya maji kwa ajili ya kuboresha hali ya upatikanaji wa maji nchini. Chanzo cha maji cha mto Ruaha Mdogo ni miongoni mwa mito inayomwaga maji nchini katika kidakio cha Great Ruaha. Kutokana na umuhimu wa Mto Ruaha Mdogo na kwa lengo la kuhakikisha mto huo unatiririsha maji kwa muda wote, Wizara kupitia Bodi ya Maji ya Bonde la Mto Rufiji tayari imekamilisha kuweka mipaka ya vyanzo vya maji na taratibu za kuvitangaza katika Gazeti la Serikali zinaendelea. Hii ni pamoja na uanzishwaji wa Jumuiya ya Watumia Maji, utunzaji wa vyanzo vya maji, upandaji wa miti rafiki na maji pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu uhifadhi vyanzo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa shamba la miti la Sao Hill lililopo Wilaya ya Mufindi, shamba hili limehifadhiwa na Wakala wa Misitu (TFS) ambapo hakuna shughuli zozote za kibinadamu zinazoendelea.