Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 1 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 3 2021-03-30

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA Aliuliza:-

Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya michezo ya kubahatisha maarufu kama bonanza kulipiwa kodi ya shilingi laki moja tu kwa mwezi na kutolipa Service Levy kwa Halmashauri?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Musukuma Joseph Kasheku, Mbunge wa Geita, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, michezo ya kubahatisha hapa nchini inasimamiwa na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania kupitia Sheria ya Michezo ya Kubahatisha, Sura Namba 41 ya mwaka 2003. Sheria hii inatambua kuainisha michezo mbalimbali ya kubahatisha ikiwemo michezo ya slot machines na imeainisha kodi na tozo iliyopaswa kulipwa kwa kuzingatia aina ya mchezo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, biashara ya michezo ya slot machine, maarufu kwa jina la bonanza, inalipiwa service levy ya asilimia 0.03 ya mapato ya mwaka yanayotokana na michezo hiyo. Tozo hiyo hukusanywa na mamlaka ya Serikali za mitaa. Hivyo basi michezo ya slot machine inalipiwa service levy kwa mujibu wa sheria iliyopo.