Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 126 2021-02-12

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA Aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kusambaza umeme wa REA kwenye baadhi ya vitongoji vya vijiji vya Namtumbo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Umeme nchini (TANESCO) pamoja na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kupeleka umeme katika vijiji na vitongoji nchini. Vijiji vyote 14 vilivyobaki katika Wilaya ya Namtumnbo vitapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili unaotarajiwa kuanza mwezi Februari, 2021 na kukamilika mwezi Septemba, 2022. Mradi huu utahusisha pia kupelekea umeme vitongoji vya vijiji vitakavyopelekewa umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuliarifu Bunge lako tukufu kuwa vitongoji vyote nchini vikiwemo vya Wilaya ya Namtumbo vitaendelea kupelekewa umeme kupitia miradi ya umeme vijijini kulingana na upatikanaji wa fedha.