Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 9 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 119 2021-02-12

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kuondoa kodi kandamizi kwa wafanyabiashara na kuweka kodi rafiki ili kuwasaidia kufanya biashara kwa uhuru na kulipa kodi kwa wakati na kuondokana na sintofahamu ya wafanyabiashara kukimbilia kufanya biashara nje ya nchi?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kulijulisha Bunge lako tukufu kuwa Serikali ya Awamu ya Tano haitozi kodi kandamizi. Aidha, Serikali imeendelea kuweka mazingira mazuri ya biashara ikiwa ni pamoja na kuongeza vivutio na fursa mbalimbali za uwekezaji kwa wazawa na wawekezaji kutoka nje. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kupitia na kuimarisha mifumo ya kisera, kisheria na kitaasisi kwa kutekeleza Mpango wa Kuboresha Mfumo wa Ufanyaji wa Biashara nchini (Blueprint for Regulatory Reforms to Improve the Business Environment) wenye lengo la kurahisisha mazingira ya kufanya biashara ambapo kupitia Sheria ya Fedha ya mwaka 2019/2020 ilifuta tozo na ada zisizo rafiki 54 zilizokuwa zinatozwa na wakala, taasisi na mamlaka mbalimbali za Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali imekuwa ikifanya maboresho mbalimbali kwenye viwango vya kodi kupitia Sheria ya Fedha (Finance Act) kila mwaka kwa lengo la kuongeza wigo wa ukusanyaji kodi na mapato mengine ya Serikali, kuchochea ukuaji wa biashara ndogo na za kati pamoja na kuhamasisha uzalishaji viwandani na kulinda viwanda vya ndani dhidi ya ushindani kutoka nje.