Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 8 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 109 2021-02-11

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE Aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha dhana ya elimu bure kwa kutoa elimu bure kuanzia Shule ya Msingi hadi Kidato cha Tano na cha Sita?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA Alijibu: -

Mheshimwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Bunda Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, dhana ya utoaji Elimu Msingi Bila Malipo inamaanisha kuwa mwanafunzi atasoma bila mzazi au mlezi kulipa ada wala michango ya fedha iliyokuwa inatozwa shuleni kabla ya kutolewa kwa Waraka wa Elimu Na. 5 wa mwaka 2015. Gharama hizo zote ambazo mzazi au mlezi alitakiwa kutoa kwa sasa hulipwa na Serikali.

Mheshimiwa Spika, dhana ya Elimu Bila Malipo inalenga elimu msingi. Elimu hii inaanzia Elimu ya Awali hadi Elimu ya Sekondari, Kidato cha Nne ili kuwajengea watoto wa Kitanzania misingi imara ya masomo ngazi zinazofuata na ustawi wa maisha yao kwa ujumla. Elimu ya kidato cha tano na sita nchini hutolewa kwa ushirikiano kati ya wazazi/ walezi na Serikali. Wazazi au walezi hutakiwa kuchangia ada ya shilingi 70,000 kwa wanafunzi wa shule za bweni na shilingi 20,000 kwa wanafunzi wa shule za kutwa kwa mwaka. Serikali hugharamia gharama nyingine zilizobaki kama vile mishahara ya walimu, vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa mfano vitabu na vifaa vya maabara pamoja na ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya shule. Ahsante.