Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 6 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 83 2021-02-09

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itamaliza kipande cha barabara kutoka Mbagala Zakhem hadi Mbagala Kuu na kipande cha barabara toka Mbande – Kisewe hadi Msongola?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Jafari Chaurembo, Mbunge wa Jimbo la Mbagala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mbagala Zakhem – Mbagala Kuu yenye urefu wa kilometa 5.1 ni miongoni mwa barabara ambazo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Awamu ya Nne alitoa ahadi mwaka 2017/2018. Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ilijenga kilometa moja ya lami katika barabara hii ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipande cha barabara ya Mbande – Kisewe – Msongola ni sehemu ya barabara ya Chanika – Mbande – Mbagala Rangi Tatu yenye urefu wa kilometa 29.4 inayounganisha barabara ya Kilwa na barabara ya Nyerere. Kati ya kilometa 29.4 kilometa 22.8 zimekwishajengwa kwa kiwango cha lami na kilometa 6.06 zilizobaki zipo kwenye kiwango cha changarawe. Barabara hii inasimamiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS).

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa kipande cha barabara kutoka Msongola mpaka Mbande kilometa 6.06 kwa kiwango cha lami. Ujenzi unaendelea kwa awamu kupitia fedha za maendeleo ambapo kuanzia mwaka 2018/2019 hadi mwaka 2020/2021 jumla ya shilingi bilioni 1.05 zimetumika kujenga kilometa moja kwa kiwango cha lami nyepesi. Kazi hiyo imeanza Msongola kuelekea Mbande. Ahsante.