Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 69 2021-02-08

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa maji kwenye Vijiji vya Engutukoiti, Losineni, Juu, Losineni kati, Oldonyawasi, Lemanda, Lemengrass, Oldonyosambu, Likurat, Olkeejulbendet, Lenigjape, Olkokula, Lemanyati, Lenjani, Seuri, Ekenywa na Ngaramtoni na Kata za Kimyak, Sambasha Tarakwa, Oloirien, Kiranyi, Likidingla, Sokon II, Olturito, Bangata, Mlanganini, Nduruma, Bwawani, Oljoro na Lahni Musa, Kisango, Mwandet Wilayani Arumeru?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lemburis Saputi Mollel, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli vijiji hivi vilikuwa na changamoto ya huduma ya maji, lakini kuanzia mwezi Disemba, 2020, Vijiji vya Lengijave, Olkokola, Seuri, Ekenywa na Ngaramtoni vimeanza kupata huduma ya maji kutoka kwenye mradi uliofadhiliwa na Shirika la Uingereza la DFID kupitia Shirika la Water Aid Tanzania. Aidha, Vijiji vingine vya Oldonyosambu, Oldonyowasi, Lemanda, Losinani Kati na Juu na Ilkuroti vinatarajiwa kupata huduma ya maji kutoka kwenye mradi huu kupitia upanuzi unaofanywa na Mamlaka ya Majisafi na Mazingira Jiji la Arusha kutoka kwenye tanki la maji lililopo kijiji cha Lengijave, lenye ukubwa wa mita za ujazo 450. Kijiji cha Lemanyata kina huduma ya maji kupitia Mradi wa Olkokola – Mwandeti.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2020/ 2021, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 1.13 kwa Wilaya ya Arumeru kwa ajili ya kuendelea na utekelezaji wa miradi ya maji katika vijiji mbalimbali. Miradi hiyo ni pamoja na ukarabati wa Mradi wa Maji wa zamani wa Nduruma – Mlangarini na kukarabati Mtandao wa Bomba unaopeleka maji Vijiji vya Themi ya Simba, Kigongoni na Samaria na ukarabati wa Mradi wa Manyire – Maurani – Majimoto utakaonufaisha Vijiji vya Maurani, Manyire na Maji moto kuwa na maji ya uhakika na Miradi ya Likamba na Oloitushura & Nengungu.