Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 68 2021-02-08

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA Aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa mradi mkubwa wa maji Chunya Mjini na kata za jirani utaanza kutekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Masache Kasaka, Mbunge wa Jimbo la Chunya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto inayoukabili Mji wa Chunya. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, hatua mbalimbali za muda mfupi na mrefu zimeendelea kuchukuliwa. Kwa upande wa muda mfupi, Serikali imejenga mradi wa uboreshaji huduma ya maji katika Mji Mdogo wa Chunya uliogharimu kiasi cha shilingi milioni 946.8. Kazi zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa tanki la ukubwa wa mita za ujazo 500, ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilometa 10.49. Mradi umekamilika kwa asilimia mia moja mwaka 2019 na umesaidia kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 36 hadi 51.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa hatua za muda mrefu, Serikali kupitia Wizara ya Maji ina mpango wa ujenzi wa mradi mkubwa wa maji kwa ajili ya wananchi wa Mji wa Chunya. Mradi huo utatekelezwa kupitia fedha za mkopo kiasi cha dola za Marekani milioni 500 kutoka Serikali ya India kupitia Benki ya Exim kwa ajili ya miji 28 Tanzania Bara na Zanzibar. Kwa sasa mradi upo katika hatua ya manunuzi ya Wakandarasi wanaotarajiwa kuwepo eneo la mradi kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi ifikapo Aprili, 2021 na ujenzi wa miradi unatarajiwa kuchukua miezi 24. (Makofi)