Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 65 2021-02-08

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACKLINE K. ANDREA Aliuliza:-

Je, Serikali imeweka mpango gani wa elimu ya sheria ya usalama barabarani kwa madereva wa bodaboda ili waendeshe kwa kutii sheria na kuepusha ajali?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako na kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jackline Kainja Andrew, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi kwa kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani limekuwa likitoa elimu kuhusu Sheria ya Usalama Barabarani kwa madereva, bodaboda na watumiaji wengine wa barabara na vyombo vya moto kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Usalama Barabarani (The Road Traffic Act No.68/1973).

Mheshimiwa Spika, elimu hiyo hutolewa kwa kupitia Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani, televisheni, radio, magazeti, vipeperushi mbalimbali, Maadhimisho ya Saba Saba na Nane Nane, matamasha mashuleni na kwenye vijiwe na maskani ya bodaboda. Aidha, katika kipindi cha kuanzia Januari mpaka Desemba, 2020 jumla ya vipindi 399 vya Elimu ya Usalama Barabarani vimerushwa hewani na kuoneshwa mubashara kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na vituo 89 vya radio na televisheni. Pia elimu imetolewa kwa madereva wa bodaboda 638,275 na kwenye vijiwe vya bodaboda 7,760 nchi nzima.

Mheshimiwa Spika, Wizara inashukuru sana wadau mbalimbali katika kutoa elimu hiyo ambayo ni TRA, PUMA, AAT, APEC, Future World Training College na Amend. Lengo ni kujenga ufahamu wa sheria na kuepusha ajali kwa madereva wa bodaboda na watumiaji wengine wa barabara. Ahsante.