Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 5 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 63 2021-02-08

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO Aliuliza: -

Serikali imeongeza viwango vya tozo za utalii kwa Hifadhi zilizo chini ya TANAPA kuanzia mwezi Julai, 2021.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kusitisha tozo hizo ili kutoa fursa kwa Sekta ya Utalii nchini ambayo imeathirika sana na ugonjwa wa Corona?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ongezeko la tozo limelenga Hifadhi za Taifa nne ambazo ni Ziwa Manyara, Serengeti, Tarangire na Arusha. Kiwango cha tozo kilichoongezeka kwa hifadhi husika ikilinganishwa na viwango vya sasa ni kama ifuatavyo: -

HIFADHI ENTRYFEE SEASONAL ANDSPECIALCAMPING FEE CONCESSIONFEE
Tozoya sasa Tozokuanzia 1/7/2021 Tozoyasasa Tozo kuanzia 1/7/2021 Tozoya sasa Tozo kuanzia 1/7/2021
Serengeti 60USD 70USD 50USD 60USD 50USD 60USD
Manyara 45USD 50USD 50USD 60USD 40USD 40USD
Tarangire 45USD 50USD 50USD 60USD 40USD 40USD
Arusha 45USD 50USD 50USD 60USD 40USD 40USD

Mheshimiwa Spika, wakati wafanyabiashara ya utalii wakiishinikiza Serikali kuacha tozo zikiwa za chini sana, wenyewe wamekua wakiwatoza watalii tozo za juu ambazo hawataki kuziweka wazi kwa Serikali. Usiri wa tozo za makampuni binafsi unainyima Serikali taarifa za msingi za kuweza kuona uzito wa hoja yao.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa rai kwamba suala la COVID-19 lisitumike kuinyima Serikali mapato ambayo yanasaidia kukuza uchumi wa nchi. Pia, nisisitize kwamba pamoja na shinikizo la kupunguza tozo, sekta binafsi haijawasilisha takwimu zozote Serikalini za kuthibitisha ongezeko la idadi ya wageni waliofuta safari zao kuja nchini kutokana na ongezeko la tozo.