Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 53 2021-02-05

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS Aliuliza:-

Jimbo la Igalula lina jumla ya vijiji 58, ambapo Vijiji 12 vimepata umeme na vijiji 46 bado havijapata umeme:-

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katika vijiji 46 ambavyo havijapata umeme?

(b) Je, gharama za kuunganisha umeme kwa kila mwananchi ni kiasi gani?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daud Protas Venant, Mbunge wa Igalula, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vilivyobaki 46 katika Jimbo la Igalula vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA awamu ya III mzunguko wa pili unaoanza katikati ya mwezi Februari 2021. Mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha miezi 18 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba, 2022. Kukamilika kwa utekelezaji wa mradi huo, kutafanya vijiji vyote katika Jimbo la Igalula kupatiwa umeme.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, katika hatua ya kuongeza kasi ya kutoa huduma ya umeme nchini mwaka 2019, Serikali kupitia TANESCO ilipunguza bei ya kuunganisha huduma ya umeme kwa wananchi wanaoishi vijijini na maeneo yanayofanana na hayo kutoka wastani wa shilingi 725,000/= kwa mita za njia tatu (three phase) hadi shilingi 139,000/= ikiwa ni punguzo la asilimia 80. Vilevile kwa mita za njia moja (single phase) kutoka wastani wa shilingi shilingi 177,000/= hadi shilingi 27,000/= sawa na punguzo la asilimia
84.75. Kwa ujumla, gharama hizo ni tozo ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).