Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 3 Water and Irrigation Wizara ya Maji 37 2021-02-04

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO Aliuliza: -

Kata za Gera, Ishozi, Ishunju, Kanyigo, Kashenye, Bwanjai, Bugandika, Kitobo, Buyango na Ruzinga katika Jimbo la Nkenge zina shida kubwa ya maji licha ya kwamba zipo kwenye mwambao wa Ziwa Victoria.

Je, ni lini Serikali itawafikishia wananchi wa kata hizo maji kutoka Ziwa Victoria kama inavyofanya kwa mikoa mingine inayopata maji kutoka katika ziwa hilo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge wa Nkenge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2020/2021 Serikali inaendelea kutekeleza miradi ya maji katika vijiji 32 ambapo imetenga jumla ya shilingi bilioni 2.084 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji katika Wilaya ya Misenyi.

Aidha, Wilaya ya Misenyi inatarajiwa kunufaika na Mradi wa Maji wa Maziwa Makuu kupitia Ziwa Victoria ambapo Mtaalam Mshauri anaendelea na usanifu wa kina unaotarajiwa kukamilika mwezi Mei, 2021 na ujenzi wa mradi kuanza mwaka wa fedha 2021/2022. Vijiji 11 vitanufaika ambavyo ni Ishunju, Luhano, Katolerwa, Kyelima, Kashenye, Bushango, Kigarama, Bweyunge, Bukwali, Kikukwe na Bugombe.