Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 2 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 21 2021-02-03

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO Aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuyagawa kwa wananchi mashamba makubwa yanayomilikiwa na wawekezaji katika Kata za Daa na Oldeani, Wilayani Karatu ambayo hayaendelezwi huku wananchi wakikosa ardhi kwa ajili ya makazi?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI Alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, ni mara yangu ya kwanza kusimama toka Bunge la Kumi na Mbili limeanza, naomba unipe fursa na mimi nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya njema, lakini nimshukuru sana Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuniamini tena katika kipindi hiki cha pili, kunipa dhamana ya kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Aidha, niwashukuru Wanailemela wote walionipa fursa hii ya kuweza kuwatumikia kwa miaka mingine mitano na kwa leo nitoe pole kwa msiba mkubwa wa Mkuu wa Shule ya Bwiru, shule ya ufundi, Ndugu Elias Kuboja ambaye amefariki dunia. Nawapa pole Wanailemela.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba sasa nijibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshinia Naibu Spika, Serikali imekuwa ikifanya kazi ya uhakiki na ukaguzi wa mashamba makubwa nchini ili kubaini uzingatiwaji wa masharti ya umiliki yaliyotolewa. Hatua zilizochukuliwa na Serikali ni pamoja na kubatilisha milki za mashamba ambayo wamiliki wamekiuka masharti ya uendelezaji. Katika kipindi cha miaka mitano (2015 – 2020) jumla ya mashamba 45 yenye jumla ya ekari 121,032.243 yalibatilishwa kutokana na waliokuwa wamiliki kushindwa kutekeleza masharti ya umiliki.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kata za Daa na Oldeani Wilaya ya Karatu, kuna mashamba 25 ambayo yalimilikishwa kwa wawekezaji kwa ajili ya shughuli mbalimbali hususan kilimo na ufugaji. Taarifa za awali za uhakiki zinaonesha kuwa mashamba hayo yameendelezwa kwa viwango tofauti ambapo mashamba tisa yameendelezwa kwa wastani wa asilimia 50. Sehemu nyingine ya mashamba hayo imejengwa miundombinu ya barabara na huduma za jamii kama vile shule, nyumba za kulala wageni, viwanda, vituo vya watalii na kadhalika. Kwa sasa Serikali inaendelea kufanya uhakiki wa kina wa mashamba yote na kuchukua hatua kwa wamiliki ambao wameshindwa kutimiza masharti ya umiliki.