Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 2 2021-02-02

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza:-

Je, ni lini Shule ya Sekondari Isike iliyopo katika Kata ya Igombe itafunguliwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rehema Juma Migilla, Mbunge wa Ulyankulu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Shule ya Sekondari Isike ilijengwa katika makazi ya wakimbizi kwa lengo la kuhudumia wakimbizi na watoto wa jamii inayowazunguka. Mwaka 2012, Serikali ilitoa maelekezo kwa wakimbizi wote waliokuwa wanaishi katika Kambi ya Ulyankulu warejee kwa hiari nchini kwao. Katika kutekeleza agizo hilo, wakimbizi walirejea makwao na wachache waliomba uraia na kuendelea kuishi katika maeneo hayo, hivyo shule ilibaki na wanafunzi wachache sana.

Mheshimiwa Spika, Serikali iliamua kuwahamisha wanafunzi waliobaki na kuwapeleka katika Shule ya Sekondari Ulyankulu. Kwa kifupi, kufungwa kwa shule hiyo kulitokana na kuzingatia matumizi sahihi ya rasilimali watu, fedha na vifaa pamoja na mazingira salama na bora kwa wanafunzi kujifunzia.

Mheshimiwa Spika, hadi sasa wanafunzi wa eneo hilo wamepelekwa na kupangwa katika Shule ya Sekondari Ulyankulu. Serikali itafungua Shule ya Sekondari Isike kama itabainika kuna mahitaji. Ahsante sana.