Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 53 2020-04-08

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:-

Kijiji cha Segoma Wilayani Mkinga ni miongoni mwa vijiji vitakavyopata umeme wa REA III.

Je, kwa nini Serikali isitumie fursa hiyo kuunganisha umeme katika Sekondari ya Lanzoni iliyopo karibu na Kitongoji cha Darajani?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula, Mbunge wa Mkinga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) inatoa kipaumbele kupeleka umeme katika Taasisi za umma na za kijamii ikiwa ni pamoja na Shule za Awali, Msingi na Sekondari, Vyuo vya Ufundi Stadi, Vituo vya Afya, Zahanati, Visima vya Maji na Nyumba za Ibada.

Mheshimiwa Naibu Spika, Katika Mwaka wa fedha 2019/2020 Serikali kupitia TANESCO inaendelea na kazi ya kusambaza umeme katika Vijiji vya Mgamboshashui, Kumbamtoni na Mpale. Kazi hiyo inahusisha kupeleka umeme katika Shule za Sekondari Duga na Lanzoni zilizopo katika Jimbo la Mkinga.

Mheshimiwa Naibu Spika, Gharama ya kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivyo vitatu pamoja na shule hizo za Sekondari ni Shilingi Milioni 91. Utekelezaji wa kazi hiyo ulianza mwezi Machi, 2020 na utakamilika mwezi Mei, 2020. Jumla ya wateja wa awali zaidi ya 175 wataunganishiwa umeme.