Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 51 2020-04-08

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wadau wote wanaotumia rasilimali ya maji katika shughuli zao wanashiriki pia kikamilifu kuhifadhi vyanzo vya maji ikiwemo misitu, mabonde na ardhi?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Magdalena Hamis Sakaya, Mbunge wa Jimbo la Kaliua kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha vyanzo vya maji vinahifadhiwa, Wizara imeweka utaratibu mbalimbali ili kuhakikisha wadau wote wanaotumia rasilimali ya maji katika shughuli zao wanashiriki kikamilifu kuhifadhi vyanzo vya maji ikiwemo misitu, mabonde na ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, taratibu hizi ni pamoja na kuweka muundo wa kitaasisi wa usimamizi wa rasilimali za maji ambao unashirikisha watumia maji kupitia vyama vya watumia maji, utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji Na. 11 ya 2009 sambamba na sheria ya nyingine zinazohusika katika utunzaji wa vyanzo vya maji na kuandaa na kutekeleza mipango ya pamoja ya usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji nchini.