Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 17 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 140 2016-05-11

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:-
Sera ya Serikali ni kuzitaka Halmashauri zote nchini kutenga fedha kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Vijana na Akina Mama kwa mujibu wa sheria ili kuwezesha upatikanaji wa mikopo yenye masharti nafuu; lakini Halmashauri nyingi ikiwemo Morogoro Vijijini haitoi mikopo hiyo kwa makundi hayo kama ilivyokusudiwa:-
Je, Serikali ina mpango gani mahsusi wa kuzibana na kuziamuru Halmashauri zote ikiwemo ya Morogoro Vijijini kutenga asilimia tano ya fedha za mapato ya ndani kwa vijana na asilimia tano kwa ajili ya akina mama ili waweze kupata mikopo yenye riba nafuu na kutimiza lengo lililokusudiwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omary Tebweta Mgumba, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro imewezesha vikundi 39 vya wanawake na vijana vyenye wanachama 295 ambavyo vimepata mikopo ya shilingi milioni 23.8 kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana na Wanawake. Katika mwaka wa fedha 2015/2016, zimetengwa shilingi milioni 175, kwa ajili ya wanawake na vijana kutokana na mapato ya ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mkakati wa Serikali hivi sasa ni kuimarisha makusanyo ya mapato ili kujenga uwezo wa kutenga fedha zaidi.
Aidha, katika bajeti ya mwaka 2016/2017, sharti la kupitisha makisio ya bajeti ya kila Halmashauri lilikuwa ni kuonesha asilimia kumi zilizotengwa kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Vijana na Wanawake. Kutokana na mapato ya ndani Halmashauri zote zimeagizwa kuhakikisha fedha hizo zilizopelekwa kwenye vikundi husika ikijumuisha walemavu na kusimamia marejesho yake ili vikundi vingine viweze kunufaika.