Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 6 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 49 2020-04-08

Name

Zubeda Hassan Sakuru

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBEDA H. SAKURU aliuliza:-

Kumekuwa na vyama vingi vinavyotambuliwa kama vyama vya wasanii na wanamichezo nchini.

(a) Je, kuna jumla ya vyama vingapi halali vya wasanii na wanamichezo ambavyo vinatambuliwa kwa mujibu wa sheria?

(b) Serikali imechukua hatua gani dhidi ya vyama visivyo na usajili vya Sanaa na Michezo?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zubeda Hassan Sakuru Viti Maalum lenye sehemu A na B kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia mwezi Disemba mwaka 2019 vipo vyama 69 ambavyo vinatambuliwa kwa mujibu wa Sheria ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Na. 23 ya mwaka 1984, ikisomwa pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2019. Kwa upande wa michezo vipo jumla ya vyama 11 kwa ngazi ya kata vyama 28 vya Wilaya, Vyama 193 vya Kimkoa na Vyama 74 vya Kitaifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya BASATA namba 23 ya mwaka 1984; ikisomwa pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2019 na BMT ni kosa la jinai kwa mtu yeyote kujihusisha na shughuli za Sanaa na Michezo pasipo na usajili na vibali halali vya Serikali. Vyama vya Michezo visivyosajiliwa haviruhusiwi kushiriki kwenye michezo yoyote rasmi inayofanyika kwenye ngazi za Wilaya, Mkoa au Taifa.