Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 44 2020-04-06

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE aliuliza:-

Ileje ina miradi iliyobuniwa kwa ajili ya kuzalisha umeme wa maji Mradi wa Luswisi na Ibaba, umeme huu ukizalishwa utaiwezesha Ileje kuwa na umeme wa kutosha kwa mahitaji yake yote na ziada na kuuza:-

(a) Je, Serikali itawasaidia vipi wananchi wa Ileje katika kukamilisha miradi hii?; na

(b) Je, Serikali itawasaidia vipi kuhakikisha usambazwaji wa umeme Ileje unaharakishwa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janet Zebedayo Mbene, Mbunge wa Ileje, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuzalisha umeme wenye uwezo wa Megawati 4.7 katika eneo la Luswisi Wilayani Ileje. Gharama za mradi ni Shilingi Bilioni 19.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Umeme Ibaba unafadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kupitia Kanisa la Moraviani – Tukuyu ambapo mradi huu ulibuniwa kuzalisha umeme kupitia jua na kusambaza kwa wanakijiji. Hata hivyo, utekelezaji wa mradi ulisuasua kutokana na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kupeleka umeme wa grid katika Kijiji hicho mwaka 2017. Kwa sasa mradi huo unasambaza nishati ya umeme katika maeneo ya Shule ya Msingi Ibaba na Kituo cha Afya Ibaba.

(b) Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kuhakikisha Vijiji vyote vya Wilaya ya Ileje vinapata huduma ya umeme kupitia Miradi ya Wakala wa Umeme Vijijini (REA) awamu ya pili na awamu ya tatu inayoendelea. Utekelezaji wa miradi ya REA awamu ya tatu utakamilika mwezi Juni, 2021.