Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 37 2020-04-06

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI aliuliza:-

(a) Je serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma za Afya katika Hospitali ya Wilaya ya Tunduru na Katika Vituo vya Afya Nakapanya na Matemanga?

(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Vituo vya Afya na Zahanati katika Kata na Vijiji ili kuendana na Sera ya Afya na Ilani ya CCM?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Ramo Matala Makani, Mbunge wa Tunduru Kaskazini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na mpango wa uboreshaji wa Hospitali ya Wilaya ya Tunduru ambapo wodi mbili ziko katika hatua ya ukamilishaji kwa gharama ya Shilingi milioni 140. Aidha, Hospitali imewezeshwa kufungua duka la dawa na kupatiwa mashine ya Ultrasound. Serikali imetumia shilingi milioni 500 kukarabati Kituo cha Afya Matemanga na Shilingi milioni 200 kujenga wodi ya mama na mtoto na jengo la upasuaji katika Kituo cha Afya Nakapanya?

(b) Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mpango wa ujenzi wa Vituo vya Afya kwa awamu na tayari imekamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vitatu Wilayani Tunduru kwa gharama ya shilingi biloni 1.3 na inaendelea na ujenzi wa Kituo cha Afya Nakapanya kwa gharama ya shilingi milioni 200. Majengo mengine yaliyobaki yataendelea kupewa kipaumbele ili kufikia azima ya kusogeza huduma karibu na wananchi.