Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 36 2020-04-06

Name

Rose Kamili Sukum

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE K. SUKUM aliuliza:-

Kutokana na wingi wa watu na shughuli za kiuchumi zilizopo katika Kata ya Bassotu kama vile uchimbaji madini, uvuvi, kilimo, ufugaji na biashara na hivyo kuwa na hatari ya milipuko ya magonjwa:-

Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Wodi ya Watoto, Wanawake, Wanaume na nyumba za watumishi wa Zahanati ya Bassotu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rose Kamili Sukumu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kutokana na Mwongozo unaosimamia utoaji wa huduma za afya, zahanati hazina Wodi ya Watoto, Wanawake na Wanaume. Hata hivyo, kutokana na umbali uliopo kati ya zahanati hiyo na Hospitali ambao ni kilometa 55, Serikali itafanya tathmini ili kuboresha miundombinu iliyopo na kuifanya Zahanati ya Bassotu kuwa na hadhi ya Kituo cha Afya.