Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Madini 33 2020-04-03

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALOME W. MAKAMBA aliuliza:-

Je, ni sifa zipi ambazo mzabuni anatakiwa kuwa nazo ili kupewa nafasi ya usimamizi mapato ya Serikali kwenye migodi midogo midogo (rush) kama Mwabomba, Namba Mbili, Segese na kadhalika?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Salome Wycliffe Makamba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na Wizara katika kutenga maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo na kufungua masoko ya madini nchi nzima, kumesababisha ongezeko la wachimbaji wadogo ambao wamekuwa wakivamia maeneo mbalimbali (rush) kama vile kwenye maeneo yaliyotengwa, maeneo yenye leseni kubwa za utafiti, maeneo ya uchimbaji mkubwa, maeneo yasiokuwa na leseni na maeneo ambayo leseni zake hazijaendelezwa kwa shughuli za uchimbaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Tume ya Madini ilitoa Waraka wa Ndani Na. 3 ulioanza kutumika tarehe 15 Oktoba, 2019 wenye dhumuni la kutoa mwongozo kwa Maafisa Madini Wakazi na watumishi wengine katika kusimamia, kudhibiti shughuli za madini na mapato ya Serikali katika maeneo yenye rush. Kwa mujibu wa Waraka huo, utaratibu unaotumika kuwapata wasimamizi wa rush kama alivyouliza Mheshimiwa Mbunge, ni kupitia Kamati ya Uongozi inayofuatilia na kuimarisha usimamizi katika eneo la rush.

Mheshimiwa Spika, Kamati hiyo huteua wasimamizi wa rush ambapo Mwenyekiti wa rush anapaswa kuwa na sifa zifuatazo: Awe mchimbaji mzoefu hasa katika usimamizi wa maeneo ya aina hiyo; asiwe na historia ya wizi wa fedha za Serikali; na awe mwaminifu. Aidha, wajumbe wengine kwenye usimamizi wa rush ni pamoja na Katibu, Mweka Hazina, Mwenyekiti wa Kijiji, Mwenyekiti wa Kitongoji, Mjumbe wa REMA, TAWOMA na mwakilishi wa eneo/shamba.