Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 25 2020-04-03

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI aliuliza:-

Je Serikali inatumia sheria gani kuwahamisha wakulima kwenye maeneo ya mijini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Mipango Miji, Na.8 ya mwaka 2017 na Sheria ya Ardhi, Na.4 ya mwaka 1999, Serikali haihamishi wakulima kwenye maeneo ya mijini badala yake inazuia wananchi kujihusisha na shughuli za kilimo cha mazao marefu katika maeneo hayo. Aidha, mazao mafupi kama kilimo cha mazao ya mikunde yanaruhusiwa kulimwa maeneo ya mijini kwa kuzingatia Sheria ya Mipango Miji.