Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 17 2020-04-01

Name

Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY S. MAGERELI aliuliza:-

Ujenzi wa chujio la maji katika Bwawa la Manchira, ambalo ni chanzo pekee cha maji katika Mji wa Mugumu, Wilayani Serengeti umechukua muda mrefu sana na kusababisha wananchi kukosa amani na kupata maji yasiyokuwa na ubora kwa matumizi ya binadamu:-

(a) Je, Serikali ina kauli gani juu ya ujenzi wa chujio hilo na lini litakamilika?

(b) Je, ni lini Serikali itakamilisha mfumo wa usambazaji maji toka Bwawa la Manchira ili kuwafikishia wananchi wote wa Mji wa Mugumu na maeneo ya jirani huduma ya maji?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy Simon Magereli, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli ujenzi wa chujio katika Bwawa la Manchira umechukua muda mrefu, sababu kuu ikiwa ni upungufu uliojitokeza katika usanifu wa chujio na udhaifu katika uwezo wa kifedha wa mkandarasi aliyekuwa anatekeleza mradi huo. Kutokana na mwenendo usioridhisha wa utekelezaji, Wizara na kuzingatia ushauri wa kitaalam mnamo tarehe 8/1/2020 iliamua kuvunja mkataba wa ujenzi wa chujio hilo.

Mheshimiwa Spika, Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira Musoma (MUWASA) na Mugumu (MUGUWASA), zimeelekezwa kutathimini na kupitia gharama zinazohitajika ili kukamilisha ujenzi wa chujio hilo kwa kutumia wataalam wa ndani (Force Account). Wizara itatoa fedha zitakazohitajika kukamilisha ujenzi wa chujio hilo linalohudumia Mji wa Mugumu.

Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi wote wa Mji wa Mugumu na maeneo ya jirani, Serikali kupitia fedha za mkopo kutoka India, itakarabati na kupanua mtandao katika Mji wa Mugumu. Usanifu wa awali umefanyika ambapo kazi zitakazofanyika ni pamoja na ujenzi wa matenki mawili ya kuhifadhia maji yenye ujazo wa mita 5,000 na 500, ulazaji wa bomba zenye vipenyo mbalimbali zenye urefu wa kilomita 200 na kutoka urefu wa sasa wa kilomita 42 na ukarabati mkubwa wa bomba za sasa na uboreshaji wa chujio.