Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 12 2020-04-01

Name

Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SILAFU J. MAUFI aliuliza:-

Serikali inatambua vivutio kadhaa vya utalii ikiwemo Kalambo Falls Mkoani Rukwa. Hata hivyo, barabara ya kuelekea maporomoko hayo kutokea Kijiji cha Kawala hairidhishi.

(i) Je, Serikali ina mpango gani wa kuiboresha barabara hiyo itakayokuwa ikitumika na watalii?

(ii) Je, kwa nini kipande hiki chenye urefu wa kilometa 12 kuanzia barabara ya Kijiji cha Kawala kisiwekewe lami?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI WA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silafu Jumbe Maufi, Mbunge Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya matengenezo ya kilometa 6.5 za barabara ya Kalambo Falls kwa kiwango cha changarawe na kujenga makalvati kwa gharama ya shilingi milioni 160.8 ili kuhakikisha barabara hiyo inapitika katika kipindi chote cha mwaka.

(b) Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2020/ 2021 Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umepanga kufanya usanifu wa kina wa kipande cha barabara ya kutoka Kijiji cha Kawala hadi Kalambo Falls chenye urefu wa kilometa 12 ili kubaini gharama halisi zinazohitajika kwa ajili ya kujenga kipande hicho cha barabara kwa kiwango cha lami.