Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 1 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 5 2020-03-31

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:-

Serikali ilipata ufadhili wa kujengewa uwanja wa michezo Mkoani Dodoma kutoka Serikali ya Morocco.

Je, ni lini uwanja huu wa Michezo utaanza kujengwa?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felister Aloyce Bura, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mfalme Mohamed VI alipofanya ziara yake katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Oktoba, 2016 alitoa ahadi ya kufadhili miradi mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na ujenzi wa msikiti mkubwa na ujenzi wa uwanja wa kisasa wa michezo nchini. Baadhi ya ahadi kama ujenzi wa msikiti zimeshakamilika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ujenzi wa uwanja wa michezo wa kisasa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliamua uwanja huo ujengwe katika Jiji la Dodoma eneo la Nane Nane. Maandalizi yote ya msingi ikiwa ni pamoja na kutenga eneo lenye jumla ya ekari 328.6, kupima eneo lote la mradi, kufanya tathmini ya mazingira na kijamii (Environmental and So cial Impact Assessment), topographical survey, geotechnical survey na kuandaa mchoro wa awali wa uwanja tarajiwa yamefanywa.

Mheshimiwa Spika, kimsingi maandalizi ya awali ambayo yalipaswa kufanywa na Serikali ya Tanzania yamekamilika kwa kiasi kilichokusudiwa. Aidha, mawasiliano baina ya Serikali mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Morocco kuhusu kukamilisha mradi huu yanaendelea.