Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 1 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 2 2020-03-31

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:-

Nchi Wahisani na Wa shirika wa Maendeleo wamekuwa wakishindwa kuleta misaada na ahadi zao kwenye utekelezaji wa Bajeti ya Maendeleo kwa wakati na nyakati nyingine kushindwa kuleta kabisa katika kipindi cha miaka mitatu ya fedha mfululizo iliyopita ya 2016/2017, 2017/ 2018 na 2018/2019:-

Je, Serikali inatueleza ni kitu gani kinasababisha hali hii?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Ernest Silinde, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikishirikiana na nchi Wahisani pamoja na Washirika wa Maendeleo katika kutekeleza Bajeti yake kwa kupokea fedha za Bajeti ya Maendeleo kupitia Misaada na Mikopo nafuu kwa mujibu wa makubaliano ya kimkataba.

Mheshimiwa Spika, kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo kuanzia 2016/2017 hadi 2018/2019 Washirika wa Maendeleo wamekuwa wakitimiza ahadi zao kwa wastani wa zaidi ya asilimia 77 kwa mtiririko ufuatao:-

Mheshimiwa Spika, mw aka 2016/2017 ki asi kilichopokelewa kutoka kwa Washiriki wa Maendeleo kilikuwa ni shilingi bilioni 2,474 sawa na asilimia 69 ya lengo la kipindi hicho la kupokea shilingi bilioni 3,601; mwaka 2017/2018 kiasi kilichopokelewa kilikuwa ni shilingi bilioni 3,351 sawa na asilimia 84 ya lengo la kipindi hicho la kupokea shilingi bilioni 3,971; na mwaka 2018/2019 kiasi kilichopokelewa kilikuwa ni shilingi bilioni 2,082 sawa na asilimia 78 ya lengo la kipindi hicho la kupokea shilingi bilioni 2,676.

Aidha, katika kipindi cha kuanzia Julai, 2019 hadi Februari, 2 020 fe dha za mis aa da na mikop o nafuu zilizopokelewa kutoka kwa Washirika wa Maendeleo zimefikia jumla ya shilingi bilioni 1,631.19 sawa na asilimia 90 ya lengo la kipindi hicho.

Mheshimiwa Spika, kwa takwimu hizi, siyo sahihi hata kidogo kusema kwamba kuna nyakati nyingine Washirika wa Maendeleo wamekuwa hawatimizi ahadi zao kabisa.