Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 1 2020-03-31

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSESPH M. MKUNDI aliuliza:-

Kituo cha Afya Bwisya kimekarabatiwa na kuongezewa miundombinu muhimu kufikia kiwango cha hospitali:

Je, kwa nini Serikali isipandishe hadhi kituo hicho na kuwa Hospitali ili kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa wakazi wa visiwa vya Ukerewe?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuanzia Julai, 2017 hadi Machi, 2020 Serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 800 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya Bwisya na Muriti. Vilevile Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, alielekeza baadhi ya kiasi cha fedha za maafa ya ajali ya Kivuko cha Ukerewe kiasi cha shilingi milioni 860 zitumike kupanua na kuboresha miundombinu ya Kituo cha Afya Bwisya. Hivyo kituo hicho kimejengwa na kukarabatiwa kwa jumla ya shilingi bilioni 1.26.

Mheshimiwa Spika, Serikali inakamilisha taratibu za kukipandisha hadhi Kituo cha Afya Bwisya kilichopo kwenye Kisiwa cha Ukara ili kiwe na hadhi ya Hospitali ya Halmashauri.