Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 53 Energy and Minerals Wizara ya Madini 472 2019-06-26

Name

Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA aliuliza:-

Kumekuwa na dalili za upatikanaji wa madini ya dhahabu katika Vijiji vya Kabingo, Ruhuru, Nyakayenzi, Nyamwilonge na Muhange Wilayani Kakonko na katika baadhi ya vijiji uchimbaji umeanza:-

Je, Serikali inatoa ushauri gani kwa vijana ambao wapo tayari kujishughulisha na uchimbaji wa madini?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Christopher Kajoro Chiza, Mbunge wa Jimbo la Buyungu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kumekuwa na dalili za upatikanaji wa madini ya dhahabu katika Vijiji vya Kabingo, Ruhuru, Nyakayenzi, Nyamwilonge na Muhange, Wilayani Kakonko.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa katika Kijiji cha Nyamwilonge uchimbaji unaendelea na Serikali imekwishakutoa leseni saba kupitia Tume ya Madini, leseni za uchimbaji mdogo (primary mining licence) kwa madini ya dhahabu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mnamo mwezi Mei, 2017, Wizara ya Madini kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) ilifanya utafiti wa awali ambao uliombwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko kubaini maeneo yenye madini ya dhahabu. Katika ripoti yake ilibainika uwepo wa dhahabu katika Vijiji vya Nyakayenzi, Nyakahura na Nyamwilongo. Pia ripoti hiyo ilishauri utafiti wa kina ufanyike ili kujua kiwango cha wingi na upatikanaji wa dhahabu katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Madini inashauri vijana wote wanaotaka kujishughulisha na shughuli za uchimbaji madini kwenye maeneo hayo, wafike kwenye Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Kigoma ili waweze kupewa ushauri wa kitaalam pamoja na kuelimishwa kuhusu utaratibu wa kufuatwa kupata leseni ya uchimbaji madini ili waweze kufanya shughuli zao kwa mujibu wa sheria.