Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 53 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 466 2019-06-26

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:-

Kasi ya utekelezaji wa miradi ya REA III Jimboni Bagamoro ni ndogo:-

Je, ni lini miradi hiyo itakamilishwa katika Jimbo la Bagamoyo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, Mbunge wa Bagamoyo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea na utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Mkoa wa Pwani ambapo Bagamoyo ni miongoni mwa wilaya zinazonufaika na mradi unaoendelea kutekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, jumla ya vijiji 10 vya Jimbo la Bagamoyo vimejumuishwa katika utekelezaji wa mradi wa REA III, mzunguko wa kwanza unaoendelea. Hadi kufikia tarehe 25 Juni, 2019, vijiji vyote 10 ambavyo ni Kongo, Kimarang’ombe, Kitopeni, Kiharaka (Kiembeni na Minazi Minane), Matimbwa (Ugongomoni na Kibahengwa), Udindivu KKKT, Fukayosi, Kimele A&B, Mto wa Nyanza na Migude vimepatiwa umeme na wateja wa awali 927 wameunganishiwa umeme. Kazi inayoendelea kwa sasa ni kuunganisha wateja katika vijiji vyote vilivyotajwa kadri wanavyolipia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivyo imejumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 9.84; njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 37.14; ufungaji wa transfoma 21 za KVA 50 na 100 pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 1,154. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 2.05. Kazi ya kusambaza umeme katika mradi huu utakamilika ifikapo mwezi Juni 2020.