Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 52 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 457 2019-06-25

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA AMJADI aliuliza:-

Vituo vingi vidogo vya Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja vimefungwa na kuwapa wakati mgumu wananchi wanapohitaji huduma ya polisi wakati vilikuwa vinasaidia kupambana na uhalifu kwa wakati muafaka:-

(a) Je, ni kwa sababu gani vituo hivyo vimefungwa na wananchi kulazimika kupata huduma katika vituo vikubwa kinyume na malengo ya kuanzishwa kwake?

(b) Je, ni kwa nini vituo vya Kilimani, Mkunazini, Mlandege pamoja na vituo vingine vimefungwa na wananchi kulazimika kufuata huduma umbali mrefu?

(c) Je, hatua ya kufunga vituo hivyo inasaidia vipi katika kupambana na uhalilfu hasa katika maeneo ya katikati ya mji wa Zanzibar na Serikali ina mpango gani na majengo yake?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, Vituo vya Polisi vimegawanyika katika madaraja matatu, ambayo ni Daraja A, B na C. Utendaji kazi wa vituo hivi unazingatia Kanuni za Kudumu za Jeshi la Polisi (POG). Mathalani, kwa mujibu wa PGO 287(2), vituo Daraja A na B vinatakiwa kufunguliwa na kufanya kazi saa 24 na vituo Daraja C vinatakiwa kufunguliwa na kufanya kazi saa 12 tu kuanzia saa 12.00 asubuhi hadi 12.00 jioni.

(b) Mheshimiwa Spika, vituo ambavyo havitumiki kwa sasa ikiwemo vituo vidogo vya Mwembeladu, Shaurimoyo na Forodhani inatokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu, vipaumbele kwenye mgawanyo wa rasilimali watu na kadhalika. Aidha, kwa sasa maeneo hayo ambayo yalikuwa yanahudumiwa na vituo hivyo yanahudumiwa na vituo vikuu ya polisi vilivyo karibu.

(c) Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi inapambana na vitendo vya uhalifu maeneo ya katikati ya Mji wa Zanzibar kwa kuimarisha ulinzi, misako na doria.