Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 447 2019-06-25

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. OSCAR R. MUKASA) aliuliza:-

Kata ya Biharamulo Mjini imetangazwa kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo hivi karibuni; kwa sasa kuna mahitaji makubwa ya upangaji wa ardhi na makazi hasa katika hadhi ya kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo:-

Je, Serikali ipo tayari kuwaunga mkono wananchi wa Biharamulo Mjini wakati huu ambapo wao wenyewe wanaendelea na jitihada za ndani kuhakikisha wanakuwa na upangaji wa makazi unaoendana na hadhi mpya ya Mamlaka ya Mji Mdogo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo tayari kuwaunga mkono wananchi wa Mamlaka ya Mji Mdogo Biharamulo katika upangaji wa makazi ya mji huo. Kwa kuzingatia hilo, Serikali imekamilisha michoro elfu tisa ya mipango miji yenye jumla ya viwanja 6,356 vyenye ukubwa wa ekari 8,753.7 kati ya viwanja hivyo, viwanja 2,337 vimepimwa na upimaji unaendelea kulingana na upatikanaji wa fedha. Mpango wa baadaye ni kujenga barabara ya lami yenye urefu wa mita 700 ili kuboresha utoaji wa huduma.

Mheshimiwa Spika, upangaji na upimaji wa makazi unawawezesha wananchi kupata faida mbalimbali ikiwemo kuongeza thamani ya ardhi, kupunguza migogoro ya ardhi, wananchi kupatiwa hati miliki ambazo zinawawezesha kuzitumia kupata mikopo katika taasisi za fedha na kuwawezesha wananchi kuishi kwenye makazi yaliyopangwa hivyo kurahisisha uwekaji wa huduma kama barabara, umeme na maji. Nazielekeza Mamlaka za Serikali za Mitaa kuendelea kuhamasisha wananchi na kuwashirikisha katika upangaji, upimaji na urasimishaji wa ardhi na makazi yao.