Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 51 Water and Irrigation Wizara ya Maji 438 2019-06-24

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:-

Mradi wa Maji wa Bwawani umekuwa ukisuasua kujengwa ikiwemo kuzungushiwa uzio:-

Je, ni lini mradi huo utakamilika?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makambako, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mkataba wa ujenzi wa mradi wa kuboresha huduma ya maji kwenye Mji wa Makambako ulisainiwa tarehe 23/05/2017 kati ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Iringa (IRUWASA) na Kampuni ya Ujenzi inayoitwa Building Water and Earth Works Ltd ya Jijini Dar es Salaam kwa gharama ya shilingi bilioni 1,568 ikiwa ni pamoja na kodi ya ongezeko la thamani (VAT). Kazi ya ujenzi ilianza tarehe 08/06/2017 na kwa mujibu wa mkataba, kazi hii ilitakiwa kukamilika tarehe 08/02/2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati wa utekelezaji wa mradi huu kulijitokeza kazi ya ziada ya ujenzi wa uzio kuzunguka chanzo cha maji cha bwawani ili kuzuia uchafuzi unaofanyika kwenye chanzo hicho. Kazi hii imeongeza muda wa kukamilisha kazi zilizopangwa kwa mujibu wa mkataba hadi tarehe 30/06/2019. Kwa sasa uzalishaji wa maji katika chanzo hicho unaendelea na tayari mradi huo unatoa huduma kwa wananchi. Kazi zilizobaki zitaendelea kukamlishwa huku wananchi wakiendelea kupata huduma ya maji.