Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 51 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 435 2019-06-24

Name

Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:-

Sekondari ya Lanzoni iliyopo Wilayani Mkinga ilianzishwa mwaka 1995 kwa lengo la kuchukua wanafunzi wa chaguo la pili lakini inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa umeme, maji, usafiri pamoja na makazi ya watumishi:-

Je, Serikali ina Mikakati gani ya kushirikiana na Halmashauri ya Mkinga katika kutatua changamoto hizo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yosepher Ferdinand Komba Mbunge wa Viti maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa Shule ya Sekondari ya Lanzoni ina changamoto nyingi za kimazingira ikiwemo kutokuwa na umeme wa grid, maji na uhaba wa nyumba za walimu. Pamoja na changamoto hizo, Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri kupitia Mpango wa MMES II, ilifanikiwa kujenga nyumba mbili (2) mpya za walimu, vyumba viwili vya madarasa na maabara moja ya kisasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga imefanya tathmini ya kupeleka maji katika shule ya Lanzoni kutoka katika Mto Zigi na kubaini kuwa kiasi cha shilingi milioni 7.6 zinahitajika. Halmashauri kwa kushirikiana na wadau inaendelea kutafuta fedha ili kukamilisha kazi hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Shule ya Sekondari Lanzoni haina umeme wa grid na inatumia umeme wa jua. Hata hivyo tayari imeshaingizwa kwenye Mpango wa REA III hivyo muda wowote itaunganishwa kwenye umeme wa grid Taifa, ahsante.